Friday, July 3, 2015

"TZ,Bidhaa zauzwa bila nembo ya ubora"

Soko la Tanzania limekuwa likipokea bidhaa kutoka ndani na nje ya nchi lakini baadhi ya bidhaa zinaarifiwa kuuzwa madukani huku zikikosa nembo za ubora.
Baadhi ya bidhaa hizo pia zimeonekana kuuzwa katika maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Katika maonyesho kama hayo ya biashara ya saba saba nchini Tanzania huwa ni fursa ya wafanyibiashara na wajasiriamali kuonyesha bidhaa zao mbali mbali lakini kwa wengine huwa wanatumia fursa hiyo kusambaza na kuuza bidhaa duni kwa bei ya kutupa.
katika maonyesho hayo bidhaa hizo na nyingine zinaendelea kuuzwa huku kukiwa na sheria na utaratibu kamili .

0 comments:

Post a Comment