Idara ya umoja mataifa ya kuhudumia watoto UNICEF, inaonya kwamba
mamillioni ya watoto katika taifa lililokumbwa na vita la Yemen
wanatishiwa na utapia mlo na wako katika hatari ya kukumbwa na
magonjwa mabaya yanayoweza kuzuilika kama vile surua ya homa ya mapafu.
Vita nchini Yemen vinasababisha athari mbaya kwa watoto nchini humo. Ripoti ya UNICEF inaeleza kuwa, takriban watoto 279 wameuwawa na wengine 402 kujeruhiwa tangu mwishoni mwa mwezi marchi, pale Saudia Arabia ilipoanza kampeni yake ya mashambulizi ya anga dhdi ya waasi wa Kihouthi.
Imeripotiwa kuwa watoto takriban 318 wameandikishwa kama wanajeshi, lakini inasema inaamnini idadi ya kweli ya waioandikishwa ni kubwa Zaidi.Wakati takwimu hizo zinashutusha, UNICEF inasema watoto pia wanakabiliwa na hatari za magonjwa na utapia mlo. Msemaji wa UNICEF Christof Boulierac, anasema watoto wako hatarini kupata magonjwa yanayoweza kuzuilika kwa sababu hawajapatiwa chanjo.Kwasababu ya mzozo, Boulierac anasema vituo vya afya havina umeme wala mafuta wanayohitaji kuhifadhi chanjo kwenye mahala baridi. Anasema watoto wengi pia wanakosa chanjo za kuokowa maisha kwa sababu wazazi wao mara nyingi wanakhofia mapigano kuwapeleka kupata chanjo.UNICEF inasema idadi ya watoto waliokumbwa na maambukizo ya mabaya ya magonjwa hatari ya kupumua imeongezeka maradufu hadi watoto millioni 1.3 tangu marchi. Hii inaashiria ongezeko kubwa lakutokuwa na uwezo kwa watoto kupata matibabu yanayohitajika kwasababu mahospitali na kliniki hazifanyi kazi sawa sawa.Ripoti inasema maji machafu , hali duni za usafi wa vyoo na ukosefu wa madini ya chumvi mwilini kunawaweka watoto zaidi ya millioni 2.5 katika hatari ya kupata magonjwa ya kuharisha, ambayo mara nyingi ni hatari. Boulierac anasema utapia mlo pia ni tishio linaloongezeka.
Vita nchini Yemen vinasababisha athari mbaya kwa watoto nchini humo. Ripoti ya UNICEF inaeleza kuwa, takriban watoto 279 wameuwawa na wengine 402 kujeruhiwa tangu mwishoni mwa mwezi marchi, pale Saudia Arabia ilipoanza kampeni yake ya mashambulizi ya anga dhdi ya waasi wa Kihouthi.
Imeripotiwa kuwa watoto takriban 318 wameandikishwa kama wanajeshi, lakini inasema inaamnini idadi ya kweli ya waioandikishwa ni kubwa Zaidi.Wakati takwimu hizo zinashutusha, UNICEF inasema watoto pia wanakabiliwa na hatari za magonjwa na utapia mlo. Msemaji wa UNICEF Christof Boulierac, anasema watoto wako hatarini kupata magonjwa yanayoweza kuzuilika kwa sababu hawajapatiwa chanjo.Kwasababu ya mzozo, Boulierac anasema vituo vya afya havina umeme wala mafuta wanayohitaji kuhifadhi chanjo kwenye mahala baridi. Anasema watoto wengi pia wanakosa chanjo za kuokowa maisha kwa sababu wazazi wao mara nyingi wanakhofia mapigano kuwapeleka kupata chanjo.UNICEF inasema idadi ya watoto waliokumbwa na maambukizo ya mabaya ya magonjwa hatari ya kupumua imeongezeka maradufu hadi watoto millioni 1.3 tangu marchi. Hii inaashiria ongezeko kubwa lakutokuwa na uwezo kwa watoto kupata matibabu yanayohitajika kwasababu mahospitali na kliniki hazifanyi kazi sawa sawa.Ripoti inasema maji machafu , hali duni za usafi wa vyoo na ukosefu wa madini ya chumvi mwilini kunawaweka watoto zaidi ya millioni 2.5 katika hatari ya kupata magonjwa ya kuharisha, ambayo mara nyingi ni hatari. Boulierac anasema utapia mlo pia ni tishio linaloongezeka.
"Mamillioni ya watoto Yemen watishiwa na magonjwa"