Tuesday, June 23, 2015

Shehe Zuberi Kaimu Mufti

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limemtangaza Shehe Abubakar Zuberi Ally kuwa Kaimu Shehe Mkuu na Mufti wa Tanzania kufuatia kifo cha aliyekuwa Mufti Shehe Shaaban Issa bin Simba kufariki dunia wiki moja iliyopita.
Shehe Zuberi, atashika wadhifa huo kwa siku 90 ili kupisha uchaguzi utakaofanyika kumpata kiongozi huyo mkuu wa Waislamu nchini kwa mujibu wa taratibu za Kiislamu.
Uteuzi huo ulifanyika na kutangazwa jana asubuhi Bagamoyo, Pwani mara baada ya Baraza la Ulamaa lenye wajumbe 7 kukaa na kumteua Shehe Zuberi kushika wadhifa huo.

0 comments:

Post a Comment