Paka mmoja wa Japani ambaye alipata umaarufu alipofanywa kuwa mkuu wa
kituo cha reli, amefariki, na waombolezaji wengi wamejitokeza
Wakuu na washabiki walihudhuria mazishi ya paka huyo, katika kituo cha reli, ambako alitumika.
Paka huyo aliyejulikana kwa jina ''Tama'' ambaye alipatikana akiranda randa katika kituo cha reli cha Kishi miaka minane iliyopita kabla yake kutawazwa kuwa meneja wa kituo hicho,
aliaga dunia majuzi kutokana na umri wake mkubwa wa miaka 16.
Tama aliishi katika kituo hicho akiwa amevalia sare rasmi ya afisa mkuu wa kituo cha reli na kuibuka kuwa kivutio kikubwa cha watalii.
Alivishwa kofia na kikoti maalumu alichoshonewa.
Viongozi na wananchi wa matabaka mbalimbali walimmiminia sifa paka huyo hasa wakisema kuwa ndiye aliyefufua kituo hicho cha reli.
Rais wa shirika la reli ya umeme la Wakayama Japan , bwana Mitsunobu Kojima, alimsifu Tama kwa kufufua uchumi katika eneo zima la Wakayama.
Wakuu na washabiki walihudhuria mazishi ya paka huyo, katika kituo cha reli, ambako alitumika.
Paka huyo aliyejulikana kwa jina ''Tama'' ambaye alipatikana akiranda randa katika kituo cha reli cha Kishi miaka minane iliyopita kabla yake kutawazwa kuwa meneja wa kituo hicho,
aliaga dunia majuzi kutokana na umri wake mkubwa wa miaka 16.
Tama aliishi katika kituo hicho akiwa amevalia sare rasmi ya afisa mkuu wa kituo cha reli na kuibuka kuwa kivutio kikubwa cha watalii.
Alivishwa kofia na kikoti maalumu alichoshonewa.
Viongozi na wananchi wa matabaka mbalimbali walimmiminia sifa paka huyo hasa wakisema kuwa ndiye aliyefufua kituo hicho cha reli.
Rais wa shirika la reli ya umeme la Wakayama Japan , bwana Mitsunobu Kojima, alimsifu Tama kwa kufufua uchumi katika eneo zima la Wakayama.
PAKA ALIYEHUDUMU KAMA MKUU WA KITUO CHA RELI