Shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) limepitisha azimio la kila
mchezaji wa kigeni kulipa dola 2,000 ( wastani wa milioni 5) kwa kila
msimu atakaocheza ligi kuu ya Tanzania.
Wachezaji wa kigeni waliosalia kuendelea kuchezea timu zao na wale wanaosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao watalazimika kulipa kiasi hicho cha pesa.
Msemaji na afisa habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema maamuzi ya kikao cha kamati ya utendaji ya TFF kilichoketi Jumamosi visiwani Zanzibar ni kuwa kiasi hicho cha pesa kitakuwa ni kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu nchini Tanzania.
Katika miaka ya nyuma, wachezaji wa kigeni kutoka nchi mbalimbali, hasa za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walikuwa hawatozwi kiasi chochote cha pesa licha ya kulipwa mamilioni.
Kizuguto amesema fedha hizo zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira wa miguu ujulikanao kama (Football Development Fund)
Wachezaji wa kigeni waliosalia kuendelea kuchezea timu zao na wale wanaosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao watalazimika kulipa kiasi hicho cha pesa.
Msemaji na afisa habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema maamuzi ya kikao cha kamati ya utendaji ya TFF kilichoketi Jumamosi visiwani Zanzibar ni kuwa kiasi hicho cha pesa kitakuwa ni kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu nchini Tanzania.
Katika miaka ya nyuma, wachezaji wa kigeni kutoka nchi mbalimbali, hasa za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walikuwa hawatozwi kiasi chochote cha pesa licha ya kulipwa mamilioni.
Kizuguto amesema fedha hizo zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira wa miguu ujulikanao kama (Football Development Fund)
KILA MCHEZAJI WAKIGENI KULIPA TANZANIA