Mkuu wa upelelezi nchini Rwanda,ambaye alikuwa anasakwa nchini Hispania
kwa makosa ya uhalifu wa kivita,sasa amekamatwa mjini London.
Karake alikuwa ni mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa wa Rwanda .Karake
alipigana vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Rwanda mwaka 1990 hadi
mwaka 1994 na baadaye alipata cheo cha kamanda msaidizi wa vikosi vya
kulinda Amani vya umoja wa mataifa huko Darfur. Karake ni miongoni mwa
makamanda walioko kwenye orodha ya makamanda wa Kinyarwanda wapatao 40
,waliomo katika hati ya mashitaka iliyotolewa mwaka 2008 na kikosi cha
uchunguzi cha Hispania kinachoongozwa na jaji Andreu Merelles.
No comments:
Post a Comment